• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mikataba yenye thamani ya zaidi ya bil. 22 za matengenezo ya barabara yasainiwa leo Mkoani Njombe.

Tarehe iliyowekwa: October 20th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Mikataba yenye thamani zaidi ya Bil. 22 ya ujenzi wa barabara Mkoa wa Njombe imesainiwa leo,ikiwa ni sehemu ya pili baada ya mikataba hiyo kusainiwa kwa awamu ya kwanza  Mkoani Dodoma Agosti 14, mwaka huu mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Hayo yameelezwa na Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini (TARURA) Mkoa wa Njombe,Mhandisi Gerald Matindi katika kikao cha utiaji saini mikataba ya matengenezo na ukarabati wa barabara na madaraja, awamu ya pili kwa asilimia 40,kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe.

Mhandisi Matindi,amesema kuwa lengo la kusaini mikataba hiyo kwa awamu ya pili katika ngazi ya Mkoa, baada ya ngazi ya Taifa ni kutoa umiliki wa miradi hiyo kwa  wananchi wa Mkoa wa Njombe ili waweze kupokea miradi ambayo toka miaka mitatu iliyopita imeongezeka kwa asilimia 37.

Amesema kuwa,kupitia mikataba hiyo TARURA kwa mwaka huu wa fedha, itafanikiwa kukamilisha matengenezo ya barabara zenye jumla ya kilomita 1,175.7 ambazo ni kilomita 8.9 za barabara zenye kiwango cha lami, kilomita 735.99 barabara zenye kiwango cha changarawe na matengenezo ya kawaida kilomita 430 pamoja na ujenzi wa madaraja 41. 

Aidha,amebainisha kuwa Mikataba 22 iliyosainiwa leo ni sehemu ya Mikataba 32, yenye asilimia 60 ya fedha zote zilitakiwa kutolewa katika mwaka huu wa fedha ambayo ilisainiwa Agosti 14,mwaka huu Mkoani Dodoma.

Halmashauri ya Mji Makambako imepata jumla ya Bil 2.8 ambapo bil. 1 ni fedha za tozo ya mafuta  zitazotumika katika matengenezo ya barabara ya Lumumba na barabara ya Madunda kwa kiwango cha lami  yenye urefu wa kilomita 1 zilizopo Kata ya Mwembetogwa na matengenezo kwa kiwango cha changarawe  na kifusi barabara ya mbugani na usetule yenye kilomita 12 na barabara ya Kitandililo na Wangama yenye kilomita 13.

Bil. 1 ya maendeleo ya jimbo itatumika katika matengenezo  ya barabara ya Ds na A-one kwa kiwango cha lami na jumla ya mil. 831 zitatumika katika matengenezo ya kawaida ya kilomita 166 za  barabara  na ujenzi wa madaraja 4.

Matangazo

  • Kuitwa Kwenye Usaili septemba,2025 September 04, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa