• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Waajiri hakikisheni Mikutano ya mabaraza ya wafanyakazi inafanyika-RC NJOMBE

Tarehe iliyowekwa: May 1st, 2022

Na. Lina Sanga

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Waziri Kindamba amewaagiza waajiri wa taasisi mbalimbali mkoani hapa kufanya vikao mara kwa mara na wafanyakazi kwa kushirikiana na Vyama vya wafanyakazi ili kutatua kero za wafanyakazi na kujenga umoja sehemu za kazi.

Mhe. Kindamba ametoa agizo hilo baada ya kusomwa kwa risala iliyobeba changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi wa serikali na taasisi binafsi mkoani hapa, katika sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani yaliyofanyika leo Kimkoa katika viwanja  vya polisi katika Halmashauri ya Mji Makambako na kuhudhuriwa na wafanyakazi wa sekta mbalimbali.

Amesema kuwa tabia ya baadhi ya waajiri kutofanya mabaraza ya wafanyakazi ambayo yanatakiwa kufanyika mara mbili kwa mwaka kwa ajili ya kujadili na kutatua kero na changamoto mbalimbali za watumishi,kuhakikisha wanafanya mabaraza hayo na watambue kuwa kufanyika kwa mabaraza ya wafanyakazi ni agizo ambalo kwa mara ya kwanza lilitolewa mwaka 1970 chini ya utawala wa Rais wa awamu ya kwanza wa Tanzania,hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Kuhusu madeni ya watumishi Mhe. Kindamba amesema katika mwaka wa fedha 2021/2022 mkoa wa Njombe umelipa madeni ya watumishi  jumla ya shilingi Mil.370 ikiwa ni malimbikizo ya mishahara,madai ya uhamisho na matibabu  na serikali inaendelea kulipa madeni hayo kila mara baada ya uhakiki kukamilika.

Pia Mhe. Kindamba amewaasa waajiri kulipa stahiki mbalimbali za watumishi wa sekta ya afya ikiwa ni pamoja na Malipo ya masaa ya ziada na kuitwa kazini,kwani ni haki yao kwa mujibu ya sheria hivyo kila anayestahili kulipwa alipwe.

Kuhusu uhaba wa watumishi na vitendea kazi, Mhe. Kindamba amesema kuwa Serikali inaendelea kuongeza watumishi ili waendelee kutoa huduma,na hivi sasa ajira mpya katika kada ya afya 7,612 zimetangazwa pamoja na kada ya elimu na mkoa wa Njombe pia unatarajia kupokea watumishi wapya,na kuhusu uhaba wa watumishi maeneo yenye mazingira magumu,Serikali inaendelea kuongeza watumishi maeneo  yenye mazingira magumu  ikiwemo ukanda wa ziwa nyasa kupitia utaratibu wa msawazo ndani ya  mkoa kila robo Mwaka.

Aidha,Kuhusu watendaji wasio waaminifu kunyofoa nyaraka za ofisi ili kuzuia mtumishi asipate stahiki zake,Mhe. Kindamba amewatahadhalisha watumishi au watendaji wenye tabia hiyo kuacha mara moja,na kuagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi wa malalamiko hayo na kuwachukulia hatua za kinidhamu,kwani fedha anazolipwa mtumishi hazitoki mifukoni mwao hivyo watumishi hao waache roho mbaya.

Pia ametoa wito kwa waajiri kuwaruhusu watumishi kujiunga na vyama vya wafanyakazi na kuhakikisha wanafikisha michango yao kwenye mifuko ya hifadhi za jamii kama NSSF na PSSSF,ili kuwawezesha watumishi kupata mafao yao pindi wanapostaafu na kuvitaka vyama vya wafanyakazi kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza.

Mwisho amewataka watumishi na wananchi wote mkoani Njombe kuchukua tahadhali dhidi ya maambukizi ya UKIMWI kwani takwimu za Maambukizi zipo juu sana ,lakini pia kila mwananchi ahakikishe  anapata chanjo ya Uviko 19 ili kuepuka maambukizi ya ugonjwa wa Korona, pamoja na kujiandaa kuhesabiwa katika sensa ya watu na makazi Agosti 23,2022.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Bodi ya Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere yatembelea eneo la ujenzi wa chuo hicho Makambako, Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa hususani ujenzi wa hosteli

    October 21, 2025
  • Kliniki ya ardhi yazinduliwa Mtaa wa Ilangamoto,nidhamu ya upangaji ardhi na utunzaji wa hati wasisitizwa

    October 13, 2025
  • Tuwasaidie wenye mahitaji maalum kushiriki uchaguzi 2025

    October 03, 2025
  • Kambi ya madaktari bingwa,yawapunguzia gharama wagonjwa

    September 25, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa