• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mil. 583 kujenga shule mpya ya sekondari ya Kata ya Mjimwema.

Tarehe iliyowekwa: December 14th, 2024

Na. Lina Sanga

Mil. 583 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa shule Mpya ya Sekondari ya Kata ya Mjimwema, ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule ya Makambako sekondari.

Akitoa taarifa hiyo leo Afisa elimu wa divisheni ya elimu sekondari katika Halmashauri ya Mji Makambako, Mwl. Aderick Nombo amesema kuwa, shule hiyo ya Kata ya Mjimwema itajengwa katika Mtaa wa Igangidung'u katika Kata ya Kivavi, kutokana na Kata ya Mjimwema kukosa eneo la ujenzi wa shule.

Amesema kuwa, awali Kata ya Mjimwema waliazimia kujenga shule hiyo katika eneo la shule ya Msingi Makambako, lakini imeshindikana  kutokana na eneo hilo kutokidhi vigezo.

Ametoa wito kwa wananchi wa Kata ya Mjimwema kujitoa kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo kwani licha ya kujengwa kwenye Kata ya Kivavi, wana umiliki wa shule na inatambulika kama   shule ya sekondari ya Kata ya Mjimwema na siyo Kivavi, lakini pia  wananchi wa Kata ya Kivavi watanufaika kupitia shule hiyo kwa kuwasomesha watoto wao hivyo wananchi wa Kata zote mbili wana wajibu wa kushiriki ujenzi wa shule hiyo.

Mhe. Nolasco Mlowe, diwani wa Kata ya Mjimwema ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo, na kuahidi kushiriki kusimamia mradi huo hadi utakapokamilika kwa kushirikiana na wananchi wa Kata yote ya Mjimwema.

Naye, Mwenyekiti wa Mtaa wa Igangidung'u, Nasibu Mabiki ameishukuru Serikali  kwa ujenzi wa shule hiyo katika Mtaa huo na kuahidi  kushirikiana bega kwa bega na viongozi wa Kata ya Mjimwema na wananchi kwa ujumla hadi mradi utakapokamilika , kwani maendeleo hayana Mtaa wala Kata  wananchi wa Kata na Mitaa yote   watanufaika kupitia shule hiyo.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa