• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mil. 89 zatumika kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Mtulingala, Kata ya Kitandililo,Kamati ya ujenzi ya Kijiji yapongezwa.

Tarehe iliyowekwa: May 24th, 2023

Na. Lina Sanga

Kamati ya ujenzi ya Zahanati ya  mtulingala iliyopo Kijiji cha Mtulingala Kata ya Kitandililo katika Halmashauri ya Mji Makambako, imepongezwa na Kamati ya Fedha  na Uongozi kwa usimamizi mzuri wa mradi wa ujenzi  wa Zahanati hiyo kwa viwango vinavyokubalika.

Pongezi hizo zimetolewa leo katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo ya  Kamati ya Fedha na Uongozi ya Halmashauri ya Mji Makambako,mara baada ya ukaguzi wa mradi huo ambao kwa sasa upo hatua ya ukamilishaji.

Aidha,Mhe. Rosemary Lwiva,Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako amepongeza Serikali ya Kijiji na wananchi kwa ujumla kwa kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Zahanati hiyo kwa kuchangia jumla ya Mil. 21.3 hali inayodhihirisha uhitaji wa Zahanati katika Kijiji hicho.

Pia,amewapongeza wananchi kwa  kuendelea kujitoa kufanya shughuli mbalimbali katika eneo la mradi kama uchimbaji  na ujenzi wa shimo la choo,ili kuunga mkono juhudi za Serikali za kutaka kila Kijiji kuwa na Zahanati ili kusogeza huduma za afya kwa wananchi.

Ametoa rai kwa Mkurugenzi na Menejimenti kuona namna ya kuchangia shughuli zilizobaki,ili Zahanati hiyo ianze kufanya kazi ili kuwapunguzia mwendo wananchi wa kufuata huduma za afya na na kuwapa nguvu ya kuendelea kushiriki kwenye miradi mingine zaidi. 

Mzee Onesmo Ndumbula,Mkazi wa Kijiji cha Mtulingala kwa niaba ya wananchi wa Kijiji hicho, ameishukuru Kamati ya Fedha na Uongozi   kwa kutambua kazi kubwa iliyofanywa na wananchi wa Kijiji hicho ya kujenga Zahanati na kwa  pongezi hizo wamefarijika na  imewatia moyo wa kuendelea na kazi.

Naye Mhe. Imani Fute,diwani wa Kata ya Kitandililo ametoa rai kwa Serikali kuwa,mara  baada ya kukamilika kwa ujenzi wa choo na kichomea taka, huduma za awali kama kliniki za kina mama na watoto zianze kutolewa ili  kuwapunguzia mwendo wananchi  kufuata huduma hizo.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako,Eliud Mwakibombaki amewatoa hofu wananchi wa Kijiji hicho na kuwahakikishia kuwa kwa kushirikiana na Kamati ya Fedha na Uongozi,kupitia bajeti ya mwaka 2023/2024 wataona namna ya kupata fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa Zahanati hiyo ili ianze kutoa huduma mara moja.

Mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Mtulingala uliibuliwa na wananchi  na kwa sasa upo katika hatua ya ukamilishaji, ukiwa umegharimu  jumla ya Mil. 89 ikiwa ni fedha Kutoka Serikali Kuu, Mchango wa Mbunge wa jimbo la Makambako, wananchi, wadau wa maendeleo  na Halmashauri kupitia mapato ya ndani.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa