• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Miradi yenye thamani ya Tshs, bil 4.7 imezinduliwa,kukaguliwa na kutembelewa na Mwenge wa Uhuru 2022 - halmashauri ya Mji Makambako

Tarehe iliyowekwa: April 5th, 2022

Na. Lina Sanga

Miradi sita yenye thamani ya shilingi bil. 4.7 iliyopitiwa na mwenge wa uhuru katika halmashauri ya Mji Makambako jana, imekaguliwa, kutembelewa  na kuzinduliwa  kwa kuzingatia ubora wa mradi na thamani ya fedha zilizotumika katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Miradi hiyo ni pamoja na Ujenzi wa Madarasa matatu na ofisi moja  kwa fedha za tozo za miamala ya simu katika shule ya sekondari Mlumbe iliyopo katika kata ya Lyamkena,ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami mtaa wa Soko la Mbao katika Kata ya Mjimwema,Mradi wa vijana wa kikundi cha Juhudi ambao ni wanufaika wa mkopo wa asilimia kumi inayotolewa na halmashauri katika mtaa wa Mlando,Nyumba ya mhanga wa maafa ya upepo mkali  mtaa wa Lupila katika  Kata ya Kitisi,Mradi wa kunenepesha ng’ombe,mbuzi na kondoo  mtaa wa Kihanga katika kata ya Mlowa na Ujenzi wa jengo la maabara katika kituo cha Afya Kitandililo.

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa,ndg. Sahili Geraruma amepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo lakini pia juhudi za wananchi katika kuchangia maendeleo kwenye maeneo yao na kuwataka Watendaji wa Serikali kusimamia miradi hiyo kwa ukaribu na kurekebisha kasoro ndogondogo katika baadhi ya  miradi iliyokaguliwa na Mwenge.

Aidha Geraruma amewataka vijana kuanzia miaka 18 kuunda vikundi kwa ajili ya kupata mikopo ya ailimia kumi inayotolewa na halmashauri na kuzifanyia kazi ili kukuza uchumi wa taifa, badala ya kujihusisha na vitendo viovu kama kuvuta bangi na matumizi ya dawa za kulevya,pia wanawake na watu wenye ulemavu waunde vikundi ili waweze kunufaika na mikopo inayotolewa na halmashauri zote Nchini.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Kitisi baada ya kuzindua nyumba ya Bi. Tumwihuhage Kihwele iliyojengwa na serikali baada ya bibi huyo kukosa makazi kutokana na nyumba aliyokua akiishi kubomolewa na Upepo mkali, Geraruma amesema kuwa falsafa  ya Mwenge ni kuleta tumaini mahali pasipo na matumaini,hivyo Tumwihuhage amepata tumaini jipya kupitia ujenzi wa nyumba hiyo pamoja na kitukuu chake.

Bi. Tumwihuhage ambaye ana umri zaidi ya miaka sitini ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kumjengea nyumba hiyo,na kuwa hakutegemea kumiliki nyumba hiyo pamoja na kitukuu chake kwani hana msaada wowote baada ya watoto wake wote kufariki.


Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa