• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mkoa wa Njombe wapokea Mwenge wa Uhuru leo, na utatembelea Miradi yenye thamani ya Bil. 346.5.

Tarehe iliyowekwa: April 25th, 2023

Na. Lina Sanga

Ludewa

Mwenge wa Uhuru 2023 umepokelewa leo katika Mkoa wa Njombe kutoka Mkoa wa Ruvuma, na utakimbizwa katika Halmashauri 6 za Mkoa huo kwa umbali wa 517KM na kutembelea,kukagua na kuzindua  miradi ya maendeleo 45 yenye thamani ya Bil. 346.5.

Akisoma taarifa ya Mwenge wa Uhuru mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2023,Ndg. Abdalla Shaibu Kaim ,Katibu Tawala Mkoa wa Njombe,Bi. Judica Omari kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe amesema kuwa,Mkoa huo unaendelea kutekeleza ujumbe mkuu wa  Mwenge wa Uhuru na jumbe za kudumu  kwa kusimamia utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na lishe,mapambano dhidi ya UKIMWI,mapambano dhidi ya dawa za kulevya,malaria, mapambano dhidi ya rushwa  na utunzaji wa vyanzo vya maji na mazingira.

Amesema kwa mwaka 2022,Mkoa wa Njombe umefanikiwa kupanda jumla ya miti Mil. 30  ya mbao na matunda sawa na asilimia 341 na kwa 2023 katika miezi kadhaa  jumla ya  miti Mil. 26.5 sawa na asilimia 327 imepandwa na uhamasishaji wa upandaji unaendelea hadi msimu wa mvua utakapo malizika ili kutunza vyanzo vya maji na mazingira.

Amebainisha kuwa,hadi sasa Mkoa huo una jumla ya vyanzo vya maji 3,377 na vyanzo vya maji 1,730 sawa na asilimia 50.4 vimehifadhiwa kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuweka uzio.

Aidha ,amesema kuwa kwa upande wa lishe bora jitihada mbalimbali zimeendelea kufanyika kwa kutoa elimu ya lishe kwa jamii na kuwahamasisha kula chakula bora,ili kutokomeza udumavu ambapo kwa takwimu za mwaka 2018 udumavu ulikua asilimia 53 na kwa kipindi cha mwaka 2022 udumavu umeshuka hadi asilimia 50.

Katika mapambano dhidi ya Malaria,kiwango cha Maambukizi ya ugonjwa huo ni asilimia 1.9   na jitihada mbalimbali za kutokomeza ugonjwa huo zinaendelea kufanyika kwa kutoa elimu na kinga dhidi ya malaria pamoja na ugawaji wa vyandarua kwa watoto wadogo na kina mama wajawazito.

Pia,katika mapambano dhidi ya ukatili, Bi. Judica amebainisha kuwa jumla ya mashauri 479 yaliripotiwa katika ofisi za Ustawi wa jamii na madawati ya jinsia,kati ya  mashauri hayo migogoro ya ndoa ni 223, utekelezaji wa watoto 156,ukatili wa kimwili 22,ulawiti 14 na ubakaji 15 na mashauri yote yameshughulikiws kwa mujibu wa kanuni na sheria.

Ameongeza kuwa,Mkoa wa Njombe unakabiliwa na tatizo dogo la matumizi ya bangi ,kwa vijana wenye umri kati ya miaka 17 hadi 28 na jeshi la polisi linaendelea kudhibiti matumizi ya bangi.

Kuhusu Mapambano dhidi ys rushwa jumla ya kesi 8 zilifunguliwa katika kipindi cha mwezi julai 2022,kesi 3 zilishinda,kesi 1 ilishindwa na kesi 4 zinaendelea na mapambano dhidi ya UKIMWI yamepungua kutoks asilimia 14 hadi asilimia 11.4 na Mkoa wa Njombe una jumla ya  watu 65,000 wanaoishi na Maambukizi.

Mwenge wa Uhuru utazunguka katika Halmashauri 6 za Mkoa wa Njombe kwa siku 6 na Aprili 30,utakimbizwa katika Halmashauri ya Mji Makambako na kukabidhiwa Mei mosi,2023 Mkoa wa Iringa.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa