• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mkurugenzi msaidizi wa uthibiti ubora wa elimu Wizara ya elimu,sayansi na teknolojia awapongeza wananchi wa Mbugani,Kitandililo kwa kutoa eneo la ujenzi wa shule bure

Tarehe iliyowekwa: October 3rd, 2024

Na. Lina Sanga

Mkurugenzi msaidizi wa uthibiti ubora wa elimu  Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia, Bi. Monica Mpululu amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Mbugani,Kata ya Kitandililo kwa kutoa eneo lenye ukubwa wa ekari kumi, kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ili kuwapunguzia umbali wanafunzi kuhudhuria masomo katika shule ya sekondari Mlowa na Kitandililo.

Mpululu alitoa pongezi hizo jana alipotembelea shule ya sekondari mpya ya Mbugani Kitandililo ikiwa ni ziara ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya BOOST na SEQUIP ambayo imefadhiliwa na benki ya dunia.

Amesema kuwa, wananchi waliotoa eneo hilo wameacha alama kwa vizazi vya sasa na vijavyo na kuwapongeza kwa jitihada za kuhakikisha wao wanapata elimu jirani na nyumbani na kuwataka kutunza miundombinu hiyo ili itumike muda mrefu pamoja na kuimarisha ulinzi wa watoto wa kike na kiume.

Reuben Swilla, Mratibu msaidizi wa mradi wa BOOST, Ofisi ya Rais TAMISEMI ametoa rai kwa jamii kuendelea kuhakikisha mahudhurio ya wanafunzi wa kiume yanaongezeka kwani idadi kubwa ya wanafunzi wanaoacha shule ni wanafunzi wa kiume,hali inayosababisha takwimu kuwa chini tofauti na wanafunzi wa Kike.

Julius Msigwa, kwa niaba ya wazazi wa wanafunzi katika shule hiyo na mmoja kati ya wananchi waliotoa eneo la ujenzi wa shule ameishukuru Serikali kwa ujenzi wa shule hiyo na kuahidi kuendelea kushirikiana na walimu kuhakikisha taaluma inakuwa na ulinzi wa mtoto unaimarika kwa kuhakikisha wanashughulikia matukio ya ukatili wa watoto yanayojitokeza.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako, Ndg. Kenneth Haule  ameishukuru benki ya dunia na Serikali ya awamu ya Sita kwa kuunga mkono jitihada za wananchi wa Kijiji cha Mbugani na Kitandililo kwa kutoa fedha za ujenzi wa shule hiyo, pia amewashukuru wananchi waliotoa eneo bila malipo kwa maslahi ya jamii na Watanzania kwa ujumla.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Bodi ya Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere yatembelea eneo la ujenzi wa chuo hicho Makambako, Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa hususani ujenzi wa hosteli

    October 21, 2025
  • Kliniki ya ardhi yazinduliwa Mtaa wa Ilangamoto,nidhamu ya upangaji ardhi na utunzaji wa hati wasisitizwa

    October 13, 2025
  • Tuwasaidie wenye mahitaji maalum kushiriki uchaguzi 2025

    October 03, 2025
  • Kambi ya madaktari bingwa,yawapunguzia gharama wagonjwa

    September 25, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa