• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mkutano na Mjadala ndani ya Umoja wa Mataifa kuendeshwa kwa lugha ya Kiswahili leo-Prof.Kennedy Gastorn

Tarehe iliyowekwa: July 7th, 2022

Na.Lina Sanga

Kilele cha maadhimisho ya kwanza ya siku ya kiswahili duniani leo Julai 7, 2022 uwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa utakuwa na matukio makubwa matatu, yatakayofanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.

Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa,Balozi Profesa Kennedy Gastorn ameieleza Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa,kuwa tukio la kwanza litakuwa asubuhi kuanzia saa 4 kwenye ukumbi namba 3 wa makao makuu ya  Umoja wa Mataifa, likihusisha hotuba kutoka kwa viongozi wa ngazi ya juu akiwemo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na Marais na wakuu wa nchi zinazozungumza lugha ya Kiswahili.

“Viongozi wakuu wa nchi watatoa matamko yao akiwemo Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Marais kutoka kusini mwa Afrika kama Msumbiji na Zimbabwe, tunatarajia viongozi wa Afrika Mashariki mfano Uganda na Kenya na viongozi wa mashirika makubwa kama Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO,” amesema Balozi Gastorn.

Amesema baada ya matamko ni wakati wa mjadala utakaojikita katika nafasi ya Kiswahili katika amani ya maendeleo, Wazungumzaji ni pamoja na wanazuoni, watu binafsi, sekta binafsi na viongozi wa Serikali.

Aidha  amesema kuwa licha ya mjadala huo pia watatoa maoni yao ni kwa vipi kiswahili kimekuwa ni nyenzo ya kuendeleza amani, kuunganisha watu na katika kuendeleza maisha ya watu tunapoelekea kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu "SDGS.”

"UN imepitisha azimio la matumizi ya lugha mbalimbali 'multilingualism' na lugha ya Kiswahili ni miongoni mwao,"amesema Profesa Kennedy.

Sehemu ya tatu ni maonesho ya mila na desturi za kiswahili ikiwemo mavazi, chakula na nyimbo na hili litafanyika kwenye ofisi za uwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa.

“Cha kutia moyo ni kwamba kutakuwepo na watoto wa shule ya awali  kutoka hapa Marekani ambao wanajifunza lugha ya kiswahili ,Wataonesha umahiri wao katika kiswahili na hili ni jambo la furaha kama wanavyosema wahenga kuwa ‘ngoma inayodumu ni ile inayochezwa na marika yote’ hivyo uwepo wa watoto wa shule ya awali nje ya mipaka ya Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika ni ishara nzuri kwamba kweli sasa kiswahili kinashika hatamu,” amesema Balozi Gastorn.

Ametanabaisha kuwa kwa mara ya kwanza mkutano na mjadala ndani ya Umoja wa Mataifa,utaendeshwa kwa lugha ya kiswahili kwa sababu kutakuwepo na wakalimani wa lugha zote rasmi za Umoja wa Mataifa kutoka lugha ya Kiswahili.

#jiandaekuhesabiwa2022

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa