• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mkuu wa Mkoa,Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri wasaini mikataba ya lishe Mkoani Njombe.

Tarehe iliyowekwa: October 20th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Mikataba ya lishe itayotumika kwa miaka nane imesainiwa leo Mkoani Njombe,kati ya Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya,Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Miji na Wilaya.

Akiwasilisha taarifa ya utiaji saini mikataba hiyo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Dkt. Zabron Masatu katika kikao cha utiaji saini mikataba ya lishe kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe,ambapo amebainisha kuwa Mkoa wa Njombe una asilimia 53.6 ya watoto wenye udumavu.

Amesema kuwa katika mikataba hiyo iliyosainiwa leo kuna kazi kuu mbili ambapo kazi ya kwanza ni afua ya lishe na ili kuweza kusimamia afua mbalimbali za lishe mikataba ni muhimu ili kuhakikisha wananchi hasa watoto walio chini ya miaka mitano wanapata lishe.

Dkt. Masatu amesema kuwa,moja ya afua ambazo zimekuwa zikisimamiwa sana ni kuweka mipango mizuri ya lishe kwa kutenga fedha kutoka kwenye mapato ya ndani, kulingana na idadi ya watoto wanaopatikana katika Halmashauri au Mkoa husika. ambapo kila mtoto mmoja anatengewa shilingi 1,000 kwa kila robo mwaka.

“Mfano Mkoa wa Njombe tuna watoto 110,000 kwa iyo kwenye afua hii ya lishe kila mtoto inatakiwa atengewe si chini ya shilingi 1,000 na tumekuwa tukitenga fedha hizo,jambo kubwa ambalo tunatakiwa kulisimamia ni upatikanaji wa fedha hizo na matumizi yake,kwa mwaka uliopita tulifanikiwa kwa asilimia 78 na kwa mwaka huu tunahitaji kujipanga vizuri ili tufikie asilimia 100,kwa sababu haya ni maelekezo ya Serikali na zaidi ya hilo tunahitaji kuhakikisha afya za watoto wetu hasa walio chini ya miaka mitano zinaimarika kwa ajili ya ustawi wa uchumi wan chi yetu”,alisema Dkt. Masatu.

Pia,amebainisha kuwa katika afua za afya kuna afua ya utoaji wa matone ya vitamini A kwa watoto chini ya miaka mitano na vidonge vya kuongeza damu kwa kina mama wajawazito,kwani endapo mama mjamzito ana afya sio nzuri na ana damu pungufu hata mtoto atayezaliwa atakuwa hana afya nzuri na huenda ikapelekea mama huyo kutojifungua salama na kupata matatizo hata kifo.

Aidha,Dkt. Masatu Amesema kupitia mikataba ya lishe iliyosainiwa leo,kuna afua ya watoto wanaopata chakula shuleni kupata chakula chenye vitamini,na Serikali imeanza kufanya majadiliano na wadau mbalimbali katika sekta ya biashara kuhakikisha kwenye halmashauri zote kuna wasagaji wa chakula ambao watakuwa na uwezo wa kusaga mahindi au vyakula mbalimbali na kuweka virutubisho kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi.

Judica Omari,Katibu Tawala Mkoa wa Njombe ametoa agizo kwa wakurugenzi wote wa Halmashauri kuhakikisha fedha hizo za lishe kwa ajili ya watoto zinatengwa katika bajeti kwa kila robo,na zinapatikana lakini pia amewataka Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi kuhakikisha vikao vya lishe vinafanyika kwa kuzingatia ratiba kwani ni vikao vya kisheria.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa