• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa akabidhi hundi yenye thamani ya Mil. 474.9 kwa vikundi 81 vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu.

Tarehe iliyowekwa: January 14th, 2025

Na. Tanessa Lyimo

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe.Kissa Gwakisa Kasongwa leo amekabidhi hundi yenye thamani ya Mil. 474.9 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ikiwa ni mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri ya Mji Makambako.

Mhe.Kissa akizungumza na wanufaika hao katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ukumbi wa kanisa la Romani Katoliki la Ilangamoto, amewataka wanufaika wa mikopo hiyo  kuwa waaminifu wakati wa urejeshaji, ili iweze kuwanufaisha walengwa wengine  wanaohitaji mikopo na ameipongeza Halmashauri ya Mji Makambako pamoja na madiwani kwa kusimamia na kuhakikisha fedha zilizotolewa kwa dhumuni la mikopo ya  asilimia kumi inatolewa kwa walengwa na kutotumika kwa matumizi mengine.

Naye, mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako Mhe. Hanana Mfikwa ametoa rai kwa  wanufaika kutumia mikopo hiyo katika malengo yaliyokusudiwa na sio vinginevyo, ili kuepuka usumbufu wakati wa  urejeshaji wa mikopo hiyo.

Bw.Khamis Shemababu wa kikundi cha “The Fighters” kutoka Kata ya Mjimwema, katika Mtaa wa Bwawani kwa niaba ya wanufaika wote  ameishukuru Serikali  kwa mikopo hiyo huku akitoa wito kwa vijana kuwa na tabia ya kujishughulisha kwani kwa kupitia uwajibikaji na mikopo inayotolewa na Halmashauri itawawezesha wao kuendesha maisha yao na kunufaika kiuchumi.

Halmashauri ya Mji makambako ilipokea jumla ya maombi 157 katika vikundi mbalimbali yenye thamani ya Bil 2.5 na kwa awamu ya kwanza ya utoaji wa mikopo hiyo Halmashauri imeweza kukopesha jumla ya vikundi 81 vilivyokidhi vigezo kiasi cha Mil.474.9 , vikundi vya wanawake 57 , vijana 14 na kundi la watu wenye ulemavu 10

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa