• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mtoto asiye na Sare za shule apokelewe shuleni januari 9,wasio na uwezo Mkoa na Wadau tutawatambua shuleni na kuwakamilishia mahitaji.

Tarehe iliyowekwa: January 7th, 2023


Na. Lina Sanga

Njombe

Tamko hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka januari 5,mwaka huu katika mkutano wa saba wa baraza la biashara Mkoa wa Njombe na kuwataka wazazi kukamilisha mahitaji yote muhimu ya  watoto ili waanze masomo kwa mujibu wa ratiba, na kutoa onyo kwa wafanyabiashara wanao ongeza bei ya mahitaji ya wanafunzi kiholela kuacha mara moja.

Mhe. Mtaka amesema kuwa, wapo baadhi ya watoto hawana uwezo wa kupata mahitaji ya shule kutokana na hali duni ya maisha katika familia, lakini  amepata ufaulu mzuri wa kuendelea na masomo na wengine wamefikia umri wa kuanza elimu ya awali na msingi lakini hawana uwezo wa kupata sare za shule hivyo Mkoa una jukumu la kuhakikisha watoto hao wanapata elimu bila kikwazo.

"Nyumba za nyasi zimetoa maprofesa wengi na baadhi ya  nyumba za ghorofa zimetoa matahira, hivyo ni wajibu wa Mkoa,Halmashauri na Wadau wa maendeleo katika Mkoa wa Njombe kujitoa kwa ajili ya kuwawezesha watoto wa masikini kupata elimu kwa kuwasaidia mahitaji muhimu ya shule",alisema Mhe. Mtaka.

Ametoa wito kwa walimu wakuu wa shule zote katika Mkoa wa Njombe kuwapokea watoto wasio na sare za shule ili waanze masomo yao kwa mujibu wa ratiba ya masomo , Mkoa na Halmashauri   zitawatambua watoto hao shuleni na kuwakamilishia mahitaji yao kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

Aidha,ametoa angalizo kwa Walimu Wakuu kutoweka masharti  magumu ya wanafunzi wanaotakiwa kuanza masomo,kwa kumlazimisha mzazi kununua sare za shule zaidi ya moja kwa kutozingatia hali halisi ya kiuchumi ya mzazi na kusababisha  baadhi ya wanafunzi kutopokelewa shule au kutofika shuleni kwa kutotimiza  masharti yaliyopo kwenye fomu ya maelekezo ya kujiunga na shule.

Pia, amewataka wazazi kukamilisha mahitaji ya watoto wao na Serikali haitasita kuwachukulia hatua wazazi watakao shindwa kuwatimizia mahitaji watoto kwa uzembe.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa