• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mwanaume Mwenye mke zaidi ya mmoja atahesabiwa alipolala-Ingbert Kindimba Mratibu wa Sensa Halmashauri ya Mji Makambako

Tarehe iliyowekwa: June 28th, 2022

Na.Lina Sanga

Sensa ni utaratibu wa kukusanya,kuzichambua na kuzichakata taarifa za watu katika maeneo husika kwa kutambua umri wao,viwango vyao vya  elimu,shughuli zao za kiuchumi na kijamii ambazo zinafanyika ili zisaidie Serikali,katika kuandaa Sera na Mipango ya maendeleo na kufanya tathimini ya utekelezaji wa mipango mbalimbali ambayo imewekwa.

Hayo yameelezwa na Mratibu wa Sensa Halmashauri ya Mji Makambako,Ingbert Kindimba katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika kijiji cha Kifumbe na Usetule,Kata ya Mahongole ikiwa ni sehemu ya Ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa ya Kijiji kwa Kijiji,Mtaa kwa Mtaa katika Halmashauri ya Mji Makambako.

Kindimba amesema kuwa Sensa ya watu hufanyika kila siku  katika ngazi ya familia,mama anapoandaa chakula huzingatia idadi ya watu katika kaya yake vivyo hivyo katika taifa letu,Halmashauri yetu na Vijiji vyetu ili tuweze kuandaa mipango ya maendeleo jambo la kwanza ni kupata idadi sahihi ya watu ndipo mipango iandaliwe.

Amesema kuwa mgawanyo wa pato la taifa kigezo kikuu ni idadi ya watu katika taifa,Ujenzi wa madarasa,vituo vya Afya,Zahanati na mahitaji ya dawa huzingatia idadi ya watu katika vijiji,mitaa,Kata,Mji hadi Mkoa,na idadi ya watu inapatikana kupitia zoezi la Sensa hivyo usipohesabiwa utakwamisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika eneo lako unaloishi.

Kindimba amesema kuwa Zoezi la Sensa litaanza rasmi usiku wa agosti 22 kuamkia siku ya Sensa agosti 23 hadi agosti 28 mwaka huu kwa kuzingatia mahali alipolala mtu huyo,Usiku wa kuamkia tarehe ya Sensa na taarifa za watu wote katika kaya zitatolewa na mkuu wa kaya ambaye anaaminiwa na wana kaya wengine anaweza kuwa baba,mama au mtoto wa familia husika.

“Mkuu wa Kaya sio lazima awe baba wa familia,anaweza kuwa mama au mtoto wa familia hiyo ambaye anaaminiwa na wanakaya wengine kuwa anaweza kutoa taarifa sahihi kuhusu wana kaya wengine,hivyo kwa mwanaume ambaye ana mke zaidi ya mmoja atahesabiwa alipolala usiku wa kuamkia siku ya Sensa agosti 23,kaya zingine mkuu wa kaya atakuwa mke na sio mume tena,wasafiri na watu wengine wasio na makazi maalumu watahesabiwa usiku wa kuamkia Siku ya Sensa katika maeneo walipolala inaweza kuwa nyumba za kulala wageni,vituo vya mabasi,vituo vya treni na maeneo ya masoko ambako watoto wanaoishi mitaani wanalala”,alisema Kindimba.

Ametoa wito kwa wanawake ambao wameolewa na mume mwenye mke zaidi ya mmoja kujenga uaminifu katika utoaji wa taarifa,endapo mwanaume alilala kwa mke mwingine asihesabiwe tena kwani kila mtu atahesabiwa mara moja tu,ili takwimu sahihi za watu zipatikane kwa maendeleo ya taifa,endapo taarifa zitakazotolewa hazitakuwa sahihi,athari zake kwa taifa ni za miaka kumi kwani Sensa inafanyika kila baada ya Miaka kumi hivyo mipango ya maendeleo haitaweza kutekelezwa ipasabyo.

Mwisho amewataka wananachi wote kujiandaa kuhesabiwa na kuwa tayari kutoa taarifa sahihi,kwani taarifa zote zinazotolewa ni za siri Karani atayehusika na kukusanya taarifa za watu na makazi yao,ataongozana na wajumbe wa Serikali za vijiji au Mitaa yao,kila mwana kaya ana haki ya kuhesabiwa awe mlemavu wa viungo au akili wote watahesabiwa mara moja tu.

#jiandaekuhesabiwa2022

Matangazo

  • Kuitwa Kwenye Usaili septemba,2025 September 04, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa