• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Ofisi ya Rais Ikulu kulipa gharama za Upangaji na Upimaji ardhi Makambako

Tarehe iliyowekwa: May 20th, 2022

Ofisi ya Rais ikulu kupitia Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) imeiwezesha halmashauri ya Mji Makambako kutekeleza mradi wa urasimishaji viwanja na nyumba katika mitaa miwili ambayo ni mtaa wa  Kikula katika Kata ya Makambako na mtaa wa Sekondari katika Kata ya Maguvani.

Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Urasimishaji Mijini,Mwesige Ileta alipokuwa akiutambulisha mradi huo kwa Viongozi wa mitaa ambayo itanufaika na mradi huo katika halmashauri ya Mji Makambako.

Mwesige amesema kuwa mradi huo  wa urasimishaji  katika halmashauri ya Mji Makambako utafanyika katika mitaa miwili,ambayo ni mtaa wa kikula na  mtaa wa sekondari ili kuwasaidia wananchi wote kuwa na hatimiliki.

Amesema kuwa lengo kuu la Serikali ni kuwapunguzia mzigo wananchi kwa kuwalipia gharama za upangaji na upimaji wa nyumba na viwanja,ili mwananchi ashughulike na ulipaji wa gharama za hatimiliki pekee,tofauti na sasa ambapo mwananchi anatakiwa kulipia gharama za upangaji,upimaji na hatimiliki.

Mwesige ameongeza kuwa  zoezi hilo la urasimishaji linalotarajiwa kuanza hivi karibuni,litafanyika sambamba na utoaji wa hatimiliki kwa viwanja visivyopungua elfu moja kwa watu waliolipia tu.

"Gharama za urasimishaji wa viwanja na nyumba kwa sasa ni laki moja na elfu thelathini, ambayo ni gharama ya upangaji na upimaji wa viwanja pekee, baada ya hapo inatakiwa mtu alipie gharama za hatimiliki ya kiwanja sasa ili kumpunguzia mwananchi kulipa gharama mara mbili,Ofisi ya Rais kupitia mradi wa MKURABITA imeamua kulipia gharama za upimaji na upangaji ili mwananchi alipie gharama za hatimiliki ambayo ni gharama ya mwisho",alisema Mwesige.

Amewaota hofu wananchi ambao tayari walishafanya malipo ya urasimishaji kuwa fedha zao zipo salama na zitatumika kulipia hatimiliki,na zitazobaki watarejeshewa kupitia watendaji wa mitaa ambao ndiyo wasimamizi wa akaunti hizo  kwa kushirikiana na kamati za urasimishaji za mitaa husika kwani huenda gharama zitapungua.

Aidha Mwesige amesema kuwa gharama za umilikishaji zinatofautiana kati ya kiwanja kimoja na kingine,kutokana na ukubwa au matumizi ya kiwanja husika kama ni makazi na biashara,makazi au biashara pekee.

Ametoa Wito kwa wananchi wa mtaa wa Kikula na Sekondari kuchangamkia fursa hiyo,kwani haitajirudia na wananchi wengi wanaihitaji hivyo kila mwananchi ambaye ana kiwanja au nyumba,katika mitaa hiyo ni vema kufanya malipo  kupitia akaunti za urasimishaji za mitaa yao baada ya kupewa bili wakati wa zoezi la upangaji na upimaji,ili wanufaike na mradi huo kwani hatimiliki ina faida nyingi.

Matangazo

  • Matokeo ya Kidato cha Sita Makambako Sekondari 2022 July 06, 2022
  • Tangazo la ajira Halmashauri ya Mji Makambako Juni,2022 June 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 12, 2018
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UKUSANYAJI MAPATO HALMASHAURI YA MJI MAKAMBAKO May 19, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mkutano na Mjadala ndani ya Umoja wa Mataifa kuemdeshwa kwa lugha ya Kiswahili leo-Prof.Kennedy Gastorn

    July 07, 2022
  • Hongera Halmashauri ya Mji Makambako kwa ukamilishaji wa miradi-Mkurugenzi Msaidizi OR TAMISEMI

    July 05, 2022
  • Mradi wa Ujenzi wa Machinga Complex ,Mji wa Serikali na Barabara yenye 51.2 KM Jiji la Dodoma

    July 03, 2022
  • Maafisa habari tekelezeni majukumu yenu Changamoto ni fursa

    July 03, 2022
  • Fungua

Video

TEHAMA ni Msingi wa Taifa Endelevu, Tuitumie kwa Usahihi na Uwajibikaji . Makambako TC, 2021
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa