• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Rais Samia aupongeza Mkoa wa Njombe kwa kukusanya mapato vizuri kwa mwaka 2021/2022

Tarehe iliyowekwa: August 10th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan ameupongeza Mkoa wa Njombe kwa ukusanyaji Mzuri wa mapato kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na, kuwapongeza Wakurugenzi kwa kazi nzuri waliyoifanya  na kuwataka kuendelea kuongeza juhudi katika ukusanyaji aa mapato ili kufanikisha utekelezaji wa  miradi ya maendeleo. 

Mhe. Samia ametoa pongezi hizo leo alipokuwa akihutubia wananchi wa Mkoa wa Njombe leo,katika Viwanja vya sabasaba ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe.

Kuhusu ombi la Viongozi la Mkoa wa Njombe kupandishwa hadhi kuwa Manispaa,Mhe. Samia amesema kuwa kutokana na hali ya uchumi kwa sasa ugawaji wa maeneo mapya  ya  kiutawala au kupandisha hadhi,umezuiliwa na muelekeo ni kwa wananchi,mapinduzi ya kilimo na  kunyanyua hali ya uchumi kabla ya kugawanya maeneo ya utawala.

Ameongeza kuwa kuhusu ombi la  ujenzi wa chuo kikuu katika Mkoa wa Njombe, kuna mradi wa ujenzi wa vyuo vikuu ambao unaruhusu vyuo kuweka matawi katika Mikoa,hivyo endapo kuna nafasi ya ujenzi wa chuo kikuu chochote,tawi litajengwa Njombe na endapo mradi umebana ameahidi kulifanyia  kazi kwa wakati mwingine ili kupitia mradi huo tawi la chuo kikuu lijengwe  Mkoani Njombe.

Pia, amesema kuwa kujenga mazingira ya kuwezesha kukuza uchumi kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla,miradi na mazingira ya uwekezaji inayowekwa  Viongozi wa Mikoa na Wilaya nchini ,hawana budi kubeba na kutekeleza kwa moyo mkunjufu kwani miradi mingine hujenga fursa za watanzania kufanya miradi na  shughuli zao za maendeleo,kujipatia kipato na kulipandisha taifa kwani  kujenga uchumi wa taifa unaanza chini kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja.

Ametoa wito kwa Viongozi na wananchi kuchapa kazi, kwani mazingira yanayojengwa  na ruzuku zinazotolewa ni kwa ajili ya  kufanya kazi na kuzalisha kwa tija na kwa wingi,na kuuza kwa wingi ili kupata mapato ya kutosha na kujenga taifa.

Kuhusu utawala bora,Mhe. Samia suluhu ametoa rai kwa viongozi wote kuanzia ngazi ya chini hadi Mkoa kuhudumia na kutumikia wananchi,kwani viongozi sio watawala bali  wahudumu.

"Niwaombeni twendeni tukahudumie wananchi tumewekwa na Mungu ametuteuwa tuwahudumie wananchi kwa utawala bora,kama umebahatika kukaa hapo ulipokaa mwananchi akija muhudumie vizuri kwani wananchi hawana shida,tunapowaomba kura tunatoa ahadi nyingi sana tunapopata kura tunawageuka, twende tuwahudumie wananchi",amesema Mhe. Samia.

Mwisho ametoa wito kwa watanzania wote kujitokeza kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya watu na Makazi, inayotarajiwa kuanza agosti 23, mwaka huu kwa mipango endelevu ya nchi.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa