• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

RC Mtaka aitaka TARURA Mkoa wa Njombe kulinda hadhi yake kwa kusimamia miradi ya barabara vizuri.

Tarehe iliyowekwa: October 20th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa Wakala wa barabara Vijijini (TARURA),kulinda hadhi ya taasisi hiyo kwa kusimamia vizuri utekelezaji wa miradi ya matengenezo ya barabara ili kuto sababisha  kero kwa wananchi.

Mhe. Mtaka ametoa wito huo leo katika kikao cha utiaji saini mikataba ya matengenezo na ukarabati wa barabara na ujenzi wa madaraja, kwa mwaka wa fedha 2022/2023,kilichofanyika  katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe.

Amesema kuna baadhi ya wakandarasi ni wazembe na hawatekelezi kazi zao kwa wakati na kusababisha kero kwa wananchi wanaotumia barabara hizo,kama kumwaga kifusi bila kukisambaza kwa muda mrefu.

Mhe. Mtaka amesema kuwa endapo kuna Mkandarasi hana uhakika na uwezo wake wa  kazi ni vema asisaini mkataba wa kuanza kazi,kwani endapo akishindwa kukamilisha mradi ndani ya muda uliopangwa sheria itachukua mkondo wake,kwani baadhi ya wakandarasi wabovu wanasababisha ofisi na viongozi kutukanwa kwa kazi mbovu wanazofanya.

“Mkandarasi akiharibu kazi anasababisha ofisi na viongozi kutukanwa kwa uzembe wao,watu wanaanza kusema amepewa kazi na Mkuu wa Mkoa mara amepewa kazi na kiongozi wa ofisi Fulani, lakini kumbe kila mkandarasi ameomba kazi mwenyewe na endapo kama kuna mkandarasi amepata kazi kwa kupewa na mtu Fulani aseme au ametoa rushwa ndiyo amepata kazi ajitokeze ili asijehukumiwa pindi atakapoharibu kazi”.alisema Mhe. Mtaka.

Ametoa angalizo kwa wakandarasi wote kutumia fedha watakazolipwa kukamilisha kazi,kwani endapo mradi hautakamilika kwa uzembe hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Jumla ya mikataba 22 yenye thamani ya zaidi ya Bil. 22 imesainiwa leo mbele ya Mkuu wa Mkoa,Katibu Tawala Mkoa,Wakuu wa Wilaya,Makatibu Tawala wa Wilaya,Wakurugenzi,Kamati za Usalama,Viongozi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Wilaya na Mkoa,Viongozi wa dini pamoja na wataalamu kutoka Halmashauri.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Bodi ya Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere yatembelea eneo la ujenzi wa chuo hicho Makambako, Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa hususani ujenzi wa hosteli

    October 21, 2025
  • Kliniki ya ardhi yazinduliwa Mtaa wa Ilangamoto,nidhamu ya upangaji ardhi na utunzaji wa hati wasisitizwa

    October 13, 2025
  • Tuwasaidie wenye mahitaji maalum kushiriki uchaguzi 2025

    October 03, 2025
  • Kambi ya madaktari bingwa,yawapunguzia gharama wagonjwa

    September 25, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa