• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Sheria ndogo zisipingane na Sheria kubwa - Dkt. Ashatu Kijaji.

Tarehe iliyowekwa: January 5th, 2023

Na. Lina Sanga

Njombe

Waziri wa Uwekezaji,Biashara na Viwanda, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametoa rai kwa Halmashauri zote nchini kuhakikisha sheria ndogo za Halmashauri zinazotungwa , kwa ajili ya usimamizi wa masuala mbalimbali ya kiutendaji hazipingani na sheria kubwa  zilizopo ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima.

Dkt. Ashatu ametoa rai hiyo leo katika mkutano wa saba wa  baraza la biashara, Mkoa wa Njombe  lililofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe ,baada ya kuibuka kwa malalamiko ya wafanyabiashara wa mbao kutozwa ushuru wa mbao shilingi 100 hadi 200 kwa ubao badala ya asilimia 3.

 Amesema kuwa,sheria kubwa inamtaka mfanyabiashara kulipa ushuru wa mbao asilimia 3 lakini baadhi ya Halmashauri zinaendelea kumtoza mfanyabiashara shilingi 100 kwa kila ubao, ambapo ni kinyume cha sheria na ni kikwazo kwa wafanyabiashara kuendesha biashara zao kwa mujibu wa sheria.

Ameongeza  kuwa, Wizara ya Uwekezaji,Biashara na Viwanda kwa sasa inafanya marekebisho ya sheria zinazokwamisha utekelezaji wa biashara,Viwanda na uwekezaji nchini , ili kuwaondolea vikwazo wafanyabiashara kufanya biashara zao kwa uhuru na kuwataka wafanyabishara kushiriki kikao kilichoandaliwa na Wizara ya fedha na Mipango kitakachofanyika januari 11,2023 ili kuwasilisha changamoto wanazokabiliana nazo na kupatiwa ufumbuzi.

Aidha,ametoa wito kwa  wafanyabiashara wote nchini kutunza kumbukumbu za biashara zao na kuitaka Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), kuwafundisha wafanyabiashara namna bora  ya utunzaji wa kumbukumbu za biashara zao ili kutokomeza malalamiko ya kubambikiziwa kodi yanayotolewa na wafanyabiashara.

Lakini pia amesema kuwa, Wizara ya Uwekezaji,Biashara na Viwanda inafanya mawasiliano na Wizara ya fedha na Mipango kufanya marekebisho ya sheria ya kodi ili utekelezaji wa tamko la Rais alilolitoa Mkoani Kagera la kutokukusanya kodi za nyuma ufanyike.

Pia ametoa rai kwa wafanyabiashara nchini kuwa waaminifu katika biashara wanazozifanya ikiwa ni pamoja na wakulima wa parachichi,kwa kutokuuza parachichi ambazo hazijakomaa vizuri ili kutoharibu soko la bidhaa hiyo adhimu duniani kwa sasa ,kwani Serikali imefanya jitihada kubwa ya kutafuta masoko ili kuwainua wakulima na wafanyabishara wa hapa nchini.

 

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa