• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

TASAF imenifanya niache pombe,sasa namiliki nyumba ya bati na kufuga nguruwe.

Tarehe iliyowekwa: November 18th, 2022

Na. Lina Sanga

Kauli hiyo imetolewa na Bi. Roida Mposola mwenye umri wa miaka 60 mkazi wa kijiji cha Mawande,Kata ya Utengule katika Halmashauri ya Mji Makambako ambaye ni mnufaika anayefadhiliwa na  Mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) tangu 2015.

Bi. Roida ambaye ni mjane amesema kuwa,mwaka 2017 kupitia TASAF alipewa nguruwe wawili, jike na dume ambao aliweza kuwafuga na kuzalisha kwa  awamu tatu na kufanikiwa kupata fedha ambazo zilimuwezesha kujenga nyumba ya tofali baada ya nyumba yake ya awali iliyojengwa kwa udongo kubomoka kutokana na mvua.


                                                                                                                                  Nguruwe wanaofugwa na Bi. Roida Mposola.

“Walipokuja  kuandikisha kunusuru kaya masikini mvua ilikuwa imenyesha na ndani kumelowa kwa sababu ilikuwa inavuja hata sehemu ya kuweka viti wakae watu wawili haikuwezekana,baada ya kupata msaada wa TASAF na kupewa fedha za kujikimu kila baada ya miezi miwili niliweza kujikusanya kidogo kidogo na kuwekeza kwenye kikundi cha maendeleo cha TASAF cha kuweka na kukopa cha  hapa kijijini na kufanikiwa kuanza ujenzi wa nyumba ya tofali na kuezeka bati”,alisema Bi. Roida.

                                                                                                               Nyumba ya Bi. Roida aliyoijenga baada ya kuwezeshwa na TASAF.



                                                                                                                        Nyumba ya awali ya Bi. Roida ambayo ilibomoka kabla ya kufikiwa na TASAF 2015.

Aidha amebainisha kwamba,Mwaka 2017  TASAF ilimpa mradi wa ufugaji wa nguruwe wawili jike na dume, ambapo alifanikiwa kupata vitoto 19 kwa awamu tofauti,awamu ya kwanza nguruwe huyo alizaa vitoto saba ambavyo aliuza kila kimoja kwa shilingi 50,000,awamu ya pili alizaa vitoto 6,awamu ya tatu vitoto sita ambavyo aliuza kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa nyumba ambapo mwaka 2017 nguruwe mkubwa aliuzwa shilingi 250,000 na  vitoto shilingi  50,000.

“Baada ya kukabidhiwa hao nguruwe hata pombe niliacha nilikuwa nashinda vilabuni kulewa lakini nilijiuliza Serikali na TASAF wamenionaje mimi na sio wenzangu wenye hali kama yangu?, kutoka moyoni niliamua kuacha pombe  na kuanza kuwatunza nguruwe niliopewa na nilifanikiwa kupata vitoto 7 kwa uzao wa kwanza nikauza vyote na kuanza kuwekeza kwa ajili ya tofali na bati kwa sasa namiliki nyumba nzuri na mpango wangu kwa sasa ni kujenga choo cha kisasa na jiko”,alisema Bi. Roida.

Ametoa shukurani kwa  Serikali kupitia TASAF kwa kumuwezesha kumiliki nyumba ya bati  na kupitia ufugaji wa nguruwe  na utengenezaji wa vyungu anapata fedha za kumsomesha mjukuu wake  na kuendesha maisha.

                                        Baadhi ya vyungu vinavyotengenezwa na Bi. Roida ambavyo huuza kuanzia 500 na kupata fedha za kujikimu kimaisha.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa