• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Ufunguzi wa maonyesho ya utalii karibu kusini 2022 wafanyika leo,watanzania waagizwa kudhibiti majanga ya moto.

Tarehe iliyowekwa: November 9th, 2022

Na. Lina Sanga

Iringa

Watanzania wametakiwa kuungana na kukumbushana kuhusu uchomaji moto kiholela hasa nyakati za uandaaji mashamba,kwa kutafuta  njia mbadala za kuandaa  mashamba badala ya moto ili kutunza na kuhifadhi vivutio vya utalii pamoja na misitu.

Rai hiyo imetolewa leo na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe Dkt.Pindi Chana(Mb) katika ufunguzi wa maonyesho ya utalii karibu kusini 2022, yanayofanyika Mkoani Iringa.

Mhe. Chana amesema kuwa Moto ni changamoto kubwa sana katika uhifadhi wa misitu na vivutio vya utalii kwani unasababisha uharibifu mkubwa kwa muda mfupi,na kuwataka watanzania wote kushiriki kudhibiti hasara za moto kwa kuacha kuchoma mashamba ovyo.

Amesema kuwa Serikali inatumia gharama kuvitangaza vivutio vya utalii ili kuzalisha ajira kwa watanzania na kuongeza pato la taifa,hivyo ni wajibu wa kila mwananchi kuwa mlinzi wa mwenzake juu ya matumizi holela ya moto mashambani kwa maslahi ya umma.

Pia ametoa wito kwa wananchi kuhifadhi mazingira na kutunza vyanzo vya maji ili kukabiliana na ukosefu wa maji kwa kutopitisha mifugo kwenye vyanzo hivyo na kufanya shughuli za kibinadamu ikiwamo kilimo na kuilinda misitu kuepusha jangwa kwa kudhibiti moto.

Aidha Mhe. Chana  amesema zaidi ya bil. 12 zitatumika kujenga kituo cha kutolea taarifa za utalii mikoa ya kusini katika eneo la maonyesho la utalii karibu kusini lililopo Kihese Kilolo,Mkoani Iringa kwani maonyesho hayo ni utekelezaji wa mikakati ya Serikali kufungua utalii Mikoa ya Kusini mwa Tanzania.

Ametoa wito kwa watanzania na wawekezaji wa nchi zingine kuwekeza katika mikoa ya Kusini kwa ujenzi wa hoteli zenye hadhi ya kimataifa,ujenzi wa kambi kwa kutumia hema na huduma nyingine muhimu kama chakula cha asili ili kuwavutia watalii na kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Kliniki ya ardhi yazinduliwa Mtaa wa Ilangamoto,nidhamu ya upangaji ardhi na utunzaji wa hati wasisitizwa

    October 13, 2025
  • Tuwasaidie wenye mahitaji maalum kushiriki uchaguzi 2025

    October 03, 2025
  • Kambi ya madaktari bingwa,yawapunguzia gharama wagonjwa

    September 25, 2025
  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa