• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Utaratibu wa mama mjamzito kupata huduma ya kliniki hadi aende na mwenza wake utazamwe upya - DC Kissa Gwakisa Kasongwa.

Tarehe iliyowekwa: October 20th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Utaratibu wa mama mjamzito kufika kliniki pamoja na mwenza wake ili aweze kupata huduma,ni moja ya chanzo cha baadhi ya watoto kukosa lishe tangu wakiwa tumboni.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe,Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa katika kikao cha utiaji saini mikataba ya lishe kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe, ambapo imedaiwa kuwa Mkoa wa Njombe una asilimia 53.6 ya watoto wenye udumavu.

Mhe. Kissa amesema kuwa, utaratibu uliowekwa katika vituo vya kutolea afya kumtaka mama mjamzito kufika na mwenza wake kliniki,ndipo ahudumiwe ni kikwazo kikubwa kwa baadhi ya wanawake  hasa kwa  waliobakwa na wenye wenza ambao hawaeleweki au waliozaa na waume  za watu,hali inayopelekea kina mama wengi kutofika kliniki hadi wanapojifungua na kupata huduma za msingi kwa manufaa yao na watoto walio tumboni.

Mhe. Kissa amesema ipo haja ya utaratibu huo kutazamwa kwa namna nyingine ili wanawake waweze kufika kliniki,na kupewa elimu ya lishe na kupata huduma nyingine muhimu kwa mama mjamzito ikiwa ni pamoja na kupima afya na Wilaya ya Njombe utaratibu huo umeanza kutizamwa upya ili kupunguza kikwazo cha mama mjamzito kupata huduma za kliniki.

Aidha,ameongeza kuwa licha ya sababu mbalimbali zilizobainishwa kusababisha udumavu katika Mkoa wa Njombe,Mhe. Kissa amesema kuwa ipo haja ya tafiti nyingine kufanyika hasa kuhusu hali ya baridi katika Mkoa wa Njombe,kwani huenda nayo ni sababu ya udumavu wa watoto kwani kama mifugo inachelewa kukua kutokana na baridi huenda hata binadamu wanaathiriwa na baridi katika ukuaji.

Ametoa wito kwa maafisa lishe kuwatumia watendaji wa mitaa na vijiji ili kupata takwimu sahihi za lishe,badala ya kuwauliza watu moja kwa moja kwani baadhi ya watu wanatoa takwimu za uongo na kuwataka wananchi kujenga mazoea ya unywaji maziwa kwa ajili ya afya zao.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Bodi ya Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere yatembelea eneo la ujenzi wa chuo hicho Makambako, Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa hususani ujenzi wa hosteli

    October 21, 2025
  • Kliniki ya ardhi yazinduliwa Mtaa wa Ilangamoto,nidhamu ya upangaji ardhi na utunzaji wa hati wasisitizwa

    October 13, 2025
  • Tuwasaidie wenye mahitaji maalum kushiriki uchaguzi 2025

    October 03, 2025
  • Kambi ya madaktari bingwa,yawapunguzia gharama wagonjwa

    September 25, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa