• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

UTEUZI

Tarehe iliyowekwa: September 12th, 2021

Pichani ni Dk Ashantu Kachwamba Kijaji ambaye ameteuliwa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri wa Habari ,Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari akichukua nafasi ya Dk, Faustine Ndugulile ambaye uteuzi wake umetenguliwa  wakati huo Mheshimiwa Rais ameihamishia idara ya Habari katika Wizara hiyo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni ,Sanaa na Michezo.

Katika historia ya Dk Ashantu Kijaji Kielimu ni pamoja na: Elimu ya Msingi alisoma Kondoa katika shule ya msingi Kalamba kati ya Mwaka 1984-1990 akijiunga na shule ya Sekondari ya wasichana Kilakala iliyopo Mkoani Morogoro kati ya Mwaka 1991-1994 kabla ya kwenda kidato cha tano na sita katika Taasisi ya Biashara Shinyanga (SHYCOM) akisoma masomo ya Biashara hii ilkuwa ni Mwaka 1995-1997.

Safari ya elimu ya juu Kijaji alinza katika chuo kikuu Mzumbe akibobea katika uchumi alisoma tangu Mwaka 1998-2001 na kutunukiwa shahada ya juu yaani (Advanced diploma) ya Mipango ya Uchumi ;Stashada hiyo ya juu ni sawa na shahada ya sayansi katika uchumi ambayo inatolewa na chuo kikuu cha Mzumbe hivi sasa.

Mara baada ya kuhitimu stashahada hiyo alipata fursa ya kuendelea na masomo ya juu nchini Norway katika chuo kikuu cha Kristiansand alifanya masomo yake chuoni hapo tangu Mwaka 2006-2008 na kutunukiwa shahada ya umahiri ya sayansi (MSc) katika usimamizi wa Biashara akajikita zaidi kwenye usimamizi wa kimataifa,lakini pia kati ya Mwaka 2008 hadi 2013 Dk Kijaji alifanya kazi kama mtafiti mwandamizi katika chuo kikuu cha Agder akiwasaidia Maprofesa katika ufundishaji na utafiti.

Mwaka 2009 hadi 2014 Dk kijaji alifanya kazi kama mhadhiri wa chuo kikuu cha Mzumbe katika mafunzo ya ushauri wa kitaalamu na ustawi hasa katika utengenezaji na uchambuzi wa Sera, Uchambuzi wa Kitaasisi, Uchumi wa kazi na Maendeleo, Usimamizi wa Kistratejia,Maendeleo ya vijijini, Usimamizi wa miradi na masuala ya ushirika wa kimataifa kwenye masuala ya uchumi.

July 2014 kukaribia uchaguzi Mkuu alikuwa Mhadhiri mwandamizi wa chuo kikuu cha Mzumbe akifundisha masomo ya uchumi na baadae kuingia katika ulingo wa siasa ambapo alichukua fomu Mwaka 2015 na kugombea ubunge katika jimbo la  Kondoa vijijini Mkoani Dodoma na kupata nafasi hiyo kuwakilisha wana kondoa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha katika serikali ya awamu ya tano iliyokuwa chini ya Hayati Dk John Joseph Pombe Magufuli alipata nafasi ya kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango na kuwa katika Baraza la Mawaziri kama Mbunge wa kuchaguliwa na Wananchi ambapo katika nafasi hiyo akiwa kama Waziri amehudumu kwa muhula wa kwanza wa serikali ya awamu ya tano na mnamo Sept 12, 2021 Dk Kijaji kwa mara nyingine ameteuliwa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Mama Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari nchini Tanzania hii inadhihirisha ni namna gani wanawake wanaweza kushika nyazifa kubwa nchini Tanzania.

Kazi iendelee.



Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa