• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Vijana kushiriki shughuli za maendeleo kwenye maeneo wanayoishi ni lazima-Mhe. Deo K. Sanga

Tarehe iliyowekwa: July 21st, 2022

Na. Lina Sanga

Vijana wametakiwa kushiriki shughuli za maendeleo katika Kata,Mitaa na Vijiji wanavyoishi,ili kuboresha huduma muhimu za kijamii kama ujenzi wa shule,zahanati na vituo vya afya kwa maslahi ya familia zao.

Wito huo umetolewa na Mbunge wa jimbo la Makambako,Mhe. Deo Kasenyenda Sanga baada ya kupokea malalamiko ya wazee wa Mtaa wa Igangidung’u katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika Ofisi za Mtaa huo.

Mhe. Sanga amesema kuwa vijana wote kuanzia umri wa miaka 18 na kuendelea,hawana budi kushiriki shughuli zote za maendeleo katika mtaa wanaoishi hata kama hawana watoto kwa sasa.

Amesema kuwa mtaa huo una changamoto ya ukosefu wa zahanati na shule ya msingi,ili Serikali ilete fedha wananchi wanatakiwa kuibua miradi ya ujenzi ndipo Serikali italeta fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo ambayo wananchi wameanza kuyajenga kwa nguvu zao.

“Kwani mimi najenga madarasa yote na shule nachangia nina watoto wanaosoma?,kwenye maendeleo hakuna cha kusema wewe una mtoto au huna mtoto maadamu unakaa kwenye eneo husika unatakiwa kushiriki kwenye shughuli za maendeleo,waliodai uhuru wa nchi hii walikuwa wachache lakini tunaofaidi ni wengi,hivyo maendeleo tutayoyafanya hapa  wataofaidi ni  vizazi vyote vya Igangidung’u vilivyopo na vijavyo hivyo suala la maendeleo ni lazima kila mtu kushiriki”, alisema Mhe. Sanga.

Ametoa wito kwa wakazi wote wa Mtaa huo kushikamana kwa pamoja na kumsikiliza Mwenyekiti wa Mtaa,na mamlaka yake ili waweze kufanya maendeleo ya shule katika mtaa huo.

Aidha,ameuagiza Uongozi wa mtaa huo kufanya mazungumzo na mmiliki wa eneo ambalo wanahitaji kujenga shule,na endapo kuna changamoto yoyote kuhusu gharama ya fidia watoe taarifa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako ili taratibu za Seriikali zifanyike na hatimaye ujenzi uanze.

Pia,amemuagiza Mtendaji wa Kata ya Kivavi kukaa na Kamati ya Maendeleo ya Kata(KAMAKA) ili kuanza mchakato wa kupata eneo, kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ili kuwapunguzia wananchi usumbufu wa kufuata huduma za afya mbali na mtaa wao.

Ziara ya Mbunge wa jimbo la Makambako,Mhe. Deo Kasenyenda Sanga leo imefanyika katika mtaa wa Malombwe,Kata ya Lyamkena na Mtaa wa Igangidung'u na Kibedange katika Kata ya Kivavi na kuzungumza na wananchi na kusikiliza kero zao,kutoa jumbe mbalimbali za Serikali ikiwa ni pamoja na bajeti ya Serikali ya mwaka 2022/2023,Sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 23,mwaka huu, mbolea ya ruzuku na kuhamasisha chanjo ya uviko 19 na jumla ya watu 66 wamepata chanjo hiyo.

#jiandaekuhesabiwa2022

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa