• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Waajiriwa wapya wa kada ya Ualimu na Afya watakiwa kuripoti vituo vya kazi kabla au ifikapo juni 11,2022

Tarehe iliyowekwa: July 2nd, 2022

Na. Lina Sanga

Dodoma

Waajiriwa wapya wa kada ya ualimu na afya wametakiwa kuripoti katika vituo vyao vya kazi  kabla au ifikapo juni 11, Mwaka huu vinginevyo nafasi hizo watapewa wengine wenye sifa.

Wito huo umetolewa  na  Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na  Serikaki za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) katika kikao kazi cha Maafisa habari wa Mikoa,Halmashauri na taasisi zilizopo Chini ya ofisi ya Rais TAMISEMI kilichofanyika leo Jijini Dodoma,katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Bashungwa amesema kuwa waajiriwa wapya wa kada ya ualimu waliopata ajira ni asilimia kumi tu,na asilimia tisini ya waombaji wamekosa nafasi hizo,kibinadamu inauma  lakini wasikate tamaa ajira zitaendelea kutangazwa

"Nitoe wito kwa waliokosa ajira wasikate tamaa waendelee kuvuta subira ajira zitaendelea kutangazwa,kazi ya kugawa riziki ni ngumu sana ajira zilipotoka tulisimamia vigezo na masharti lakini kwa sasa kuna memes zinazunguka  nimekua mzee kabisa lakini tumetenda haki yeyote anayetaka kukagua utaratibu uliofanyika aje kila kitu kipo",alisema Bashungwa.

Pia,amewataka wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano kuripoti shuleni ifikapo julai 4, vinginevyo nafasi zao watapangiwa wanafunzi wa akiba.

Ametoa wito kwa wazazi wa wanafunzi hao kuhakikisha watoto wanaripoti shuleni ndani ya muda uliopangwa,na kuanza masomo kwani wanafunzi wenye uhitaji wa nafasi hizo ni wengi.

Aidha,amewataka walimu wakuu na wakuu wa shule kutotoza michango yoyote nje ya nyaraka na miongozo ya Serikali,na hatua stahiki zitachukuliwa kwa mwalimu atayekiuka maagizo hayo.

Ametoa Wito kwa Makatibu wa wizara, wakuu wa Mikoa, wakurugenzi  na Maafisa elimu kusimamia ipasavyo suala la michango shuleni ili kuondoa sintofahamu inayoweza sababishwa na baadhi ya wakuu wa shule  na walimu wakuu  kutozingatia miongozo na nyaraka mbalimbali zinazotolewa na Serikali.

Jumla ya waajiriwa wapya wa kada ya Ualimu ni 9,800 na kada ya afya 6,876  kwa mwaka  wa fedha 2022/2023 na jumla ya nafasi 736 za kada ya afya zitatangazwa tena baada ya Kukosa waombaji  wenye sifa .

Kada hizo ni madaktari wa meno,teknolojia ya mionzi,tabibu msaidizi na tabibu wa meno.

#jiandaekuhesabiwa2022


Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa