• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wafanyabiashara wa mazao watakiwa kukamilisha maghala ifikapo juni 30,mwaka huu na magari ya viazi,matunda na ndizi kushusha bidhaa hizo Soko la Magegele na Maguvani.

Tarehe iliyowekwa: June 6th, 2023

Na. Lina Sanga

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako na Mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara ,wametakiwa kuhakikisha wafanyabiashara wa mazao na mali mbichi wanafanyia biashara zao katika maeneo yaliyoainishwa kulingana na aina ya biashara zao.

Wito huo umetolewa leo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako,Mhe. Hanana Mfikwa  katika Mkutano wa baraza la Madiwani la kuishia kipindi cha robo ya tatu(Januari – Machi) 2022/2023,uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Mji Makambako.

Mhe. Hanana amesema kuwa,Halmashauri haitatoa muda wa nyongeza tena kwa wafanyabiashara wa mazao ambao walianza ujenzi wa maghala, katika Mtaa wa Kiumba kwani muda wa nyongeza uliotolewa katika mikataba ya ujenzi wa maghala hayo unaisha Juni 30,2023 na kuwataka wafanyabiashara hao kuhakikisha wanakamilisha ujenzi ndani ya muda uliopangwa ili maghala hayo yaanze kutumika ifikapo Julai 1,mwaka huu.

Pia,amewataka wamiliki wa nyumba zinazotumika kama stoo za mazao kuzingatia barua za zuio la nyumba za makazi kutumika kama stoo za mazao,kwani madawa yanayotumika kuhifadhia mazao yana athari kubwa kwa wakazi wa nyumba hizo hususani watoto.

“Hatukatai  mtu yeyote kufanya biashara  mahali popote bali tumekataa kuweka maghala kwenye nyumba za kuishi watu,mtu yeyote ambaye hana mahali pakufanyia biashara amuone Mkurugenzi amuonyeshe mahali pakufanyia biashara ambapo ni rasmi kwa ajili ya biashara”,alisema Mhe. Hanana.

Aidha,ametoa wito kwa wafanyabiashara wa mali mbichi katika soko kuu la Makambako kushusha na kuuza bidhaa zao ,katika masoko yaliyoainishwa na Halmashauri ili kuendelea kuupanga mji kuanzia.

Mnamo Mei 25,mwaka huu Halmashauri ya Mji Makambako ilitoa tangazo la mwisho kuwataka wafanyabiashara wa mali mbichi,kuanza kushushia bidhaa kwenye masoko ya Magegele na Maguvani na mwisho wa kushusha bidhaa hizo soko kuu ilikuwa ni Mei 29,2023.

Magari yote yanayoleta ndizi na matunda yanatakiwa kushusha bidhaa hizo katika Soko la Maguvani na Viazi katika Soko la Magegele, na Mfanyabiashara hazuiliwi kuuza bidhaa zake katika masoko hayo au soko kuu.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa