• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wakala wa Misitu TFS yatakiwa kutumia TEHAMA,Kupunguza urasimu.

Tarehe iliyowekwa: January 6th, 2023

Na. Lina Sanga

Njombe

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Mhe. Anthony Mtaka kwa Wakala wa Misitu nchini(TFS), kuboresha na  kutumia Mifumo ya TEHAMA,katika utoaji wa vibali vya kusafirisha mazao ya misitu ili kupunguza urasimu na kuwawezesha wafanyabiashara kupata vibali popote na wakati wowote wanapohitaji.

Mhe. Mtaka alitoa rai hiyo jana katika Mkutano wa saba wa baraza la biashara Mkoa wa Njombe,uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe na kuhudhuriwa na Waziri wa Uwekezaji,Biashara na Viwanda,Mhe. Ashatu Kijaji baada ya kusikiliza changamoto  mbalimbali   wanazokabiliana nazo wafanyabiashara katika Mkoa huo.

Katika mkutano huo wafanyabiashara walipata fursa ya kutoa changamoto zao na ushauri kwa Serikali,ili kupata ufumbuzi wa baadhi ya vikwazo visivyo na ulazima katika sekta ya biashara ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kupata kibali cha kusafirisha mbao na kuhuisha kibali baada ya kupata changamoto ya usafiri.

Mhe.Mtaka amesema kuwa, utaratibu wa kupata kibali katika  ofisi za Wakala wa Misitu ni utaratibu uliopitwa na wakati, hivyo ni vema Wakala wa Misitu kuboresha mfumo wa utoaji wa vibali kutoka mfumo wa analogia hadi mfumo wa kidigitali ili mfanyabiashara aweze kulipia kibali wakati wowote na mahali popote na aruhusiwe kuuza soko lolote katika Mji unaosomeka kwenye  kibali cha usafirishaji.

Aidha,Mhe. Mtaka amewataka wafanyabiashara katika sekta ya usafirishaji wa daladala na bajaji, kuachana na migogoro baina yao ya kugombea wateja kwani kwa sasa hali ya maisha imebadilika na mteja ana uhuru wa kuchagua aina ya usafiri anaoutaka na sio kulazimishwa.

Naye Mbunge wa jimbo la Njombe Mjini, Mhe. Deo Mwanyika ametoa rai kwa Wizara  ya Uwekezaji, Biashara  na Viwanda kuwasaidia wakulima wa zao la chai kupata soko la uhakika, ili wakulima waweze kunufaika kwa kuuza chai kwa bei nzuri.

Pia ametoa wito kwa Serikali kuwekeza kwenye zao la parachichi mapema ili wakulima wa zao hilo baada ya miaka mitano wasipate hasara, kwani idadi ya wananchi waliohamasika kuwekeza kwenye kilimo cha parachichi inaongezeka siku hadi siku.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Uzinduzi wa Baraza la Madiwani wafanyika leo,Mhe.Salum Mlumbe achaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri kwa miaka 5

    December 04, 2025
  • Tulichokubaliana tutatekeleza, tulinde Mji wetu tusonge mbele.

    November 29, 2025
  • Watahiniwa wa mitihani ya kidato cha nne 2025 watakiwa kuwa watulivu ili wapate madaraja mazuri.

    November 15, 2025
  • Njombe hali ni shwari fanyeni biashara

    November 07, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa