• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wakazi wa Mkoa wa Njombe watakiwa kujiunga na Mfumo wa stakabadhi za Ghala kuongeza tija ya kilimo na uzalishaji wa bidhaa.

Tarehe iliyowekwa: April 20th, 2023

Na. Lina Sanga

Wakazi wa Mkoa wa Njombe  wametakiwa kuchangamkia fursa za mfumo wa stakabadhi za ghala, ili waweze kufanikiwa kupitia mazao na bidhaa wanazozalisha na kupata tija zaidi.

Wito huo umetolewa leo na Kaimu Meneja uratibu huduma wa  Bodi ya usimamizi wa stakabadhi za Ghala,Erick Temu katika kikao na Madiwani na Wataalamu wa Halmashauri ya Mji Makambako, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Temu amesema kuwa, mfumo wa stakabadhi za ghala ni mfumo wa masoko unaomuwezesha muweka mali kuweka mali kwenye ghala lenye leseni na kumuwezesha mzalishaji au mkulima  kupata soko la uhakika kupitia taarifa za mali husika zilizoandikwa na ubora wa bidhaa ambazo zinatangazwa kwa wadau wengi waliopo kwenye mfumo huo.

Amesema kuwa, mfumo huo pia  unampa nafasi mzalishaji mali hususani mzalishaji mali na mkulima mdogo,ambaye hana uwezo wa kufikisha mali zake sokoni,kufikisha mali zake sokoni kwa kutumia utaratibu wa ghala kupitia chama cha msingi,ambapo  wakulima na wazalishaji  wengine wanakusanya mali zao katika ghala la chama cha msingi na kusafirisha kwenda kwenye ghala kuu na kuingizwa katika kanzidata ya mfumo,na kila mdau ambaye yupo kwenye mfumo anaziona na bei itatangazwa na mnunuzi wa bei ya juu atapewa mzigo huo.

Ametaja manufaa ya mfumo huo kuwa ni pamoja na kuzalisha ajira kwa vijana kama kubeba mizigo,biashara ya chakula na nyumba za kulala wageni,kwani ghala linakutanisha watu wengi kutoka maeneo mbalimbali hivyo uchumi wa wakazi wa eneo husika unaongezeka na mkulima anapata manufaa kwa kupata soko la uhakika na kuuza bidhaa kwa bei nzuri.

Aidha, ameongeza kuwa,mfumo wa stakabadhi za ghala Unaleta utambuzi wa bidhaa ambao unawasaidia wazalishaji na wakulima, kutambulika sehemu wanayopatikana kwa urahisi na kuongeza wigo wa soko la bidhaa zinazozalishwa katika eneo husika.

Pia,amebainisha kuwa kukosekana kwa ghala kunasababisha  changamoto ya udhibiti wa bei ya uhakika ya bidhaa mbalimbali,hivyo mfumo wa stakabadhi za ghala utamsaidia mkulima na mzalishaji mali mdogo kupata tija katika kilimo na bidhaa anazozalisha.

Ametoa rai kwa wamiliki wa maghala ambao wanahitaji kuingia kwenye mfumo huo, kuhakikisha sehemu ambayo mazao yanahifadhiwa, hayataharibiwa au kunyeshewa  na mvua na yataweza  kuhifadhiwa kwa kiwango ambacho kinatosha uhifadhi wa eneo husika.

Bodi ya usimamizi wa stakabadhi za Ghala ni taasisi ya Wizara ya Uwekezaji,Viwanda na Biashara,yenye mamlaka ya kuhamasisha na kusimamia utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi za Ghala,ambao unawezesha mazao au bidhaa kuhifadhiwa ndani ya ghala zenye leseni.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa