• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

WANANCHI JITOKEZENI KUJIFUNZA MASUALA YA KISHERIA ILI KUEPUKA KUJIHUSISHA NA MAKOSA YA JINAI

Tarehe iliyowekwa: November 12th, 2021

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Makambako, Bi. Amina Kassim katika maadhimisho ya wiki ya msaada  kisheria,yaliyofanyika leo,katika kata ya Lyamkena,kupitia Shirika la TULILUMWI MAKAMBAKO,ambalo linajishughulisha na utoaji wa msaada wa kisheria katika halmashauri ya Mji Makambako.

Bi, Amina ambaye pia ni Mwanasheria wa halmashauri ya Mji Makambako, amesema kuwa,Jinai ni kitendo chochote kinachofanywa na mtu ambacho ni kinyume na sheria za Nchi na  haki za binadamu,kwani huhatarisha usalama wa mtu  na Mali zake,pia jinai ipo katika jamii zetu na tunaishi nayo,kwani jinai sio lazima iwe mauaji bali hata wizi wa kuku ni kosa la jinai kwasababu ni kinyume cha sheria za Nchi.

“Kuiba kuku pia ni jinai kwa sababu ni kinyume cha sheria za Nchi, Ulawiti, Ubakaji, Mauaji na vitendo vingine vinavyohatarisha usalama wa watu pia ni jinai na hukumu yake ni kifungo gerezani,na katika kila jamii jinai ipo na tunaishi nayo majumbani mwetu kwani wabakaji,wezi,wanaolawiti na wauaji wanatoka katika familia ama jamii zetu tunazoishi”,alisema Bi. Amina.

Ametoa wito kwa wananchi wote kuepukana na matendo ya jinai kwani kujua au kutokujua kuwa jambo Fulani ni kosa au sio kosa kisheria sio kinga dhidi ya sheria, bali mtu ataonekana hana hatia baada ya uchunguzi kufanyika na akithibitika ana hatia atapewa adhabu kwa mujibu wa sheria.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii katika halmashauri ya Mji Makambako,Masinde Ramadhan Masinde amesema kuwa,wakazi wengi wa Mji wa Makambako ni wasiri kutoa taarifa za ukatili zinazofanywa na watu wao wa karibu,na kusababisha ukatili kuongezeka kwani wengi wanaojihusisha na masuala ya ukatili walishafanyiwa ukatili mwanzo.

“Imekuwa ngumu sana kwa wazazi na walezi kutoa taarifa za ukatili wanaofanyiwa wao ama watoto wao,endapo aliyefanya ukatili huo ni mmoja wa familia ama ni mtu wa karibu na familia,kwa kigezo cha kuficha aibu pasipo kutambua kuwa usiri huo una madhara makubwa sana,kwani aliyefanyiwa ukatili  huweka kisasi dhidi ya mtu aliyemfanyia ukatili na kuamua kulipiza kwa wengine”, alisema Bw. Masinde.

Bw. Masinde ametoa wito kwa wananchi wote kutoa taarifa juu ya vitendo vya kikatili vinavyofanyika katika familia na jamii zao,na kutomaliza masuala ya ukatili na  migogoro ya ndoa,mirathi na mambo mengineyo kama ubakaji na ulawiti kifamilia bali kisheria,ili kuepuka athari mbalimbali zinazoweza kujitokeza, lakini pia kutenga muda wa kukaa na watoto wao ili kutambua hisia zao juu ya maisha yao ya shule na mitaani na kuwasikiliza.

“Wasikilizeni watoto wenu wanapokataa kusoma shule Fulani,kuna kuwa na sababu zinazomfanya mtoto akatae na siyo kumlazimisha kusoma shule hiyo kisa umelipa ada uliyoipata kwa shida,wasikilize watoto na jengeni urafiki na watoto wenu ili waweze kuwaambia mambo yanayowatatiza shuleni,kwani wanakutana na changamoto nyingi na wazazi mnachojali kulipa ada tu,endapo mtoto atakataa ama kwenda shule au kwa ndugu Fulani asikilizwe kwani wengine wanafanyiwa vitendo vya kikatili na watu hao,”, alisema Masinde.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Wiki ya Msaada Kisheria kitaifa kwa mwaka huu ni “MABORESHO ENDELEVU YA HAKI YA JINAI,KUIMARISHA UPATIKANAJI HAKI JINAI KWA WAKATI”.

MWISHO.

 

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa