• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wananchi wa Maguvani changamkieni fursa-Kenneth Haule Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako

Tarehe iliyowekwa: June 28th, 2022

Na. Lina Sanga

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako, Kenneth Haule amewataka wananchi wa Mtaa wa Sekondari Kata ya Maguvani,kuitumia fursa ya mradi wa  urasimishaji ardhi  unaotekelezwa na MKURABITA kupitia Ofisi ya Rais ikulu ya Upangaji na Upimaji ardhi bura na kuandaa hati miliki kwa gharama nafuu ambazo  zinaandaliwa katika  ofisi za mtaa huo na kukabidhiwa na wananchi,ili kumpunguzia mwananchi mzigo wa kulipia gharama kubwa na kutumia muda mrefu kufuatilia hati.

Haule ametoa wito huo jana wakati akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Sekondari uliopo Kata ya Maguvani ambao umefikiwa na mradi huo wa upangaji na upimaji  ardhi na kukabidhiwa hati kwa gharama nafuu.

Amesema kuwa Serikali inawajali wananchi wa halk ya chini na kuamua kuratibu mpango wa urasimishaji ardhi kwa gharama nafuu Nchini ili hata mwananchi wa hali ya Chini apimiwe ardhi yake na kukabidhiwa hati miliki kwa kulipia hati pekee na sio zoezi la upangaji na upimaji ardhi,lakini bado mwitikio   wa wananchi wa mtaa huo ni mdogo na hauridhishi.

"Ndugu zangu Serikali yetu inawajali sana wananchi wa hali ya chini,na imeamua kuleta Mradi huu ili kumpunguzia mwananchi gharama za upimaji wa ardhi na hati miliki, hivi sasa Serikali inakipia upangaji na upimaji wa ardhi wa kila mwananchi,wewe ulipimie hati miliki tena kwa gharama isiyozidi laki moja na nusu lakini bado wengine hadi sasa hawajalipia ili mchakato wa kupata hati miliki  uanze na wakabidhiwe hati zao, ni jambo la kushangaza sana na linasikitisha sana kwani katika Halmashauri yetu ya Mji Makambako ni Mitaa mingi yenye uhitaji wa mradi huu lakini kati ya mitaa 54 ni mitaa miwili tu inanufaika na bado hamtoi ushirikiano",alisema Haule.

Ametoa rai kwa wananchi wa mtaa wa Sekondari na Mtaa wa Kikula kuhakikisha wanajitoa katika kufanikisha zoezi hilo kiukamilifu  ili kuendana na hadhi ya Mji kwani haileti maana nzuri kwa wananchi wengine wenye uhitaji wa fursa hiyo ambao hawajabahatika kuipata kwenye mitaa yao.

Awali akizungumzia kuhusiana na utekelezaji wa zoezi la upimaji na urasimishaji wa ardhi katika Mtaa wa Sekondari, Msimamizi wa zoezi hilo kutoka ofisi ya Rais ikulu, Henry Tarimo amesema kuwa  mpaka sasa  watu elfu moja wamepimiwa maeneo yao katika Mtaa wa Sekondari,wananchi waliolipia ni 329 huku waliojitokeza kujua gharama zao ni watu 659.

Naye Afisa ardhi mteule katika Halmashauri ya Mji Makambako,Claudia Kipapi amewataka wananchi kutumia fursa hiyo kwani mpango huo ukipita, gharama za urasimishaji na umilikishaji wa hati zitakua ni kubwa tofauti na sasa.

Mpango wa Serikali wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Halmashauri ya Mji  Makambako unatekelezwa katika mitaa miwili  ikiwemo Mtaa wa Sekondari uliopo Kata ya Maguvani na Mtaa wa Kikula uliopo Kata ya Makambako,Serikali inamlipia kila mwananchi gharama za upangaji na Upimaji wa ardhi na jukumu la mwananchi ni kulipia gharama za kuandaliwa  hati ya kiwanja kwa gharama nafuu kulingana na  ukubwa na matumizi ya kiwanja husika.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa