• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Watanzania dumisheni umoja na kuilinda amani ya nchi kwa Maendeleo endelevu.

Tarehe iliyowekwa: December 6th, 2022

Na. Lina Sanga

Wito huo umetolewa leo na Meja Daniel Shija Mawenge,Kaimu Kamanda Kikosi cha Jeshi la Wananchi 514KJ,alipokuwa akihutubia wananchi na watumishi wa Halmashauri ya Mji Makambako waliofika kufanya usafi katika Kituo cha afya Makambako,ikiwa ni utekelezaji wa shughuli za kijamii katika wiki la Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika.

Meja Daniel amesema kuwa,Tanganyika ilipata Uhuru Mwaka 1961 kwa amani bila umwagaji damu,hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kuilinda amani ya nchi na kudumisha umoja ili nchi yetu iwe na maendeleo endelevu.

“Tanganyika ilipata uhuru bila kumwaga damu kutoka kwa wakoloni mataifa mengi yamepata uhuru kwa kumwaga damu,ndio maana hata bendera zao zina rangi nyekundu lakini bendera yetu haina rangi nyekundu, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kudumisha amani na umoja kwenye makazi yake yanayomzunguka kwa maslahi mapana ya taifa letu”,alisema Meja Daniel.

Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru kwa mwaka huu yanafanyika kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na upandaji miti,michezo,usafi wa mazingira,mashindano ya michezo na sanaa,mashindano ya uandishi wa insha kwa wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari na kufanya kongamano na mdahalo wa kujadili maendeleo endelevu ambayo Wilaya,Halmashauri na Mkoa imefikia kwa kipindi cha miaka 61 ya Uhuru.

Katika Halmashauri ya Mji Makambako Mdahalo wa kujadili maendeleo endelevu ya Halmashauri utafanyika desemba 8,2022 ,katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Makambako, ukihusisha watumishi wa Serikali na taasisi zote zilizopo katika Hlmashauri ya Mji Makambako,wazee wa mji na wananchi.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya miaka 61 ya uhuru kwa mwaka 2022 inasema"Amani na Umoja ni nguzo ya maendeleo endelevu".

Matangazo

  • Kuitwa Kwenye Usaili septemba,2025 September 04, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa