• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Watumishi watakiwa kuzitunza na kuzithamini nyumba za Serikali kwa Maslahi ya Umma.

Tarehe iliyowekwa: November 2nd, 2023

Na. Lina Sanga

Kamati ya fedha na uongozi ya Halmashauri ya Mji makambako imewataka watumishi kutunza nyumba wanazoishi ambazo zimejengwa  na Serikali kwa kuzithamini kama za kwao  na kufanya marekebisho madogo madogo inapobidi ili nyumba hizo zidumu muda mrefu.

Kamati ya fedha na Uongozi imetoa rai hiyo leo katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha kuishia robo ya kwanza(Julai- Septemba) kwa mwaka wa fedha 2023/2024 katika Kata ya Kitisi,Kitandililo na Mahongole.

Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uongozi Mhe. Hanana Mfikwa akizungumza na watumishi wawili wa Zahanati ya Kijiji cha Ibatu,ambao wataishi katika nyumba mpya pacha iliyojengwa kupitia mfuko wa kunusuru kaya masikini (TASAF) pamoja na wananchi, amewataka watumishi wote wanaokabidhiwa nyumba za Serikali kwa ajili ya kuishi kuhakikisha  wanazitunza kwani nyumba hizo ni zao hivyo hata kioo kikivunjika kununua kingine ni lazima.

Pia,Mhe. Hanana  amewapongeza wananchi wanaoshiriki katika usimamizi  na utekelezaji wa  miradi katika maeneo yao kwa niaba ya Serikali,kwa kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa wakati na kukamilika katika ubora unaoendana na thamani ya fedha zilizotolewa na Serikali.

Lakini pia,amewataka mafundi wakuu wanaotekeleza miradi ya Serikali kuhakikisha wanawalipa mafundi wanaowasaidia kazi kama vibarua kwa wakati ,ili kuepuka migogoro isiyokuwa na ulazima  na kuhakikisha wanakamilisha miradi ndani ya muda uliopangwa kwa viwango na ubora unaokubalika.

Ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha watoto wote wanapata mahitaji muhimu kwa ajili ya ustawi wa watoto ikiwa ni pamoja na kupata chakula shuleni, na kuwataka wananchi wa Kijiji cha Usetule kujitoa kusafisha mazingira ya shule ya msingi shikizi  ya Magomati kwa kung’oa visiki ili iwe rahisi kwa Wakala wa barabara Mijini na Vijijini(TARURA) kutengeneza barabara za kudumu.

Kamati ya fedha na uongozi leo imefanya ziara na kukagua miradi minne ambayo ni pamoja na kukagua miundombinu ya nyumba pacha ya Walimu shule ya sekondari Kitisi,ujenzi wa shule mpya ya sekondari Mbugani katika Kata ya Kitandililo,ujenzi wa nyumba pacha ya watumishi katika Zahanati ya Ibatu na Ujenzi wa madarasa sita na matundu 12 ya vyoo shule ya msingi shikizi Magomati.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa