• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wazazi watakiwa kushirikiana na walimu katika malezi ya wanafunzi.

Tarehe iliyowekwa: February 19th, 2024

Na. Lina Sanga

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako na Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha,Mhe. Hanana Mfikwa ametoa rai kwa wazazi kushirikiana na walimu katika malezi ya wanafunzi,kitaaluma na utunzaji wa miundombinu ya shule.

Mhe. Hanana ametoa rai hiyo leo katika ziara ya kamati ya fedha na uongozi ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Kata ya Mahongole, ambapo  Kamati hiyo ilifanya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa   vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Manga.

Akizungumza na baadhi ya wazazi ambao ni  wajumbe wa kamati za ujenzi wa mradi huo,amewataka kuwashirikisha na wazazi wengine juu ya umuhimu wa wazazi kushirikiana na walimu katika malezi ya watoto wanapokuwa shuleni na hasa namna ya utunzaji wa miundombinu ya madarasa ili yatumike kwa muda mrefu.

Amesema kuwa ipo haja kwa wazazi kufidia gharama ya kurekebisha miundombinu ya madarasa na hata madawati endapo watoto wao wameharibu,kwani kwa kufanya hivyo madarasa hayo yatatumika muda mrefu badala ya kusubiri Serikali ifanye matengenezo ambayo huenda ikachukua muda mrefu kutekelezeka.

"Niwaombe wazazi wenzangu mtoto anapovunja kioo au kuvunja dawati au kuharibu kitu chochote,gharama ijulikane na wazazi wachangie na maisha yaendelee,kwani hata nyumbani kwako ukivunja chupa ya chai unanunua nyingine kwa sababu kuna kuvunja bahati mbaya,hawa watoto wakivunja kioo wasiadhibiwe mana adhabu haifanyi kioo kuwa kizima badala yake wazazi wachangie na kuwaelimisha watoto juu ya uharibifu waliofanya",alisema Mhe. Hanana.

Aidha,ameipongeza Kamati ya Usimamizi na  Ufuatiliaji wa miradi ya Halmashauri ya Mji Makambako,kwa usimamizi mzuri wa miradi pamoja na kamati za ujenzi za wananchi wa eneo husika kwa kujitoa katika usimamizi wa miradi hadi inapokamilika.

Kamati ya fedha na Uongozi leo imetembelea miradi minne ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi Manga, Mawande, Ikwete na shule ya Msingi Makambako,shule hizo zote zilipokea fedha kiasi cha mil. 45 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa