• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wilaya ya Njombe kukusanya mapato 100% ifikapo Juni,2023.

Tarehe iliyowekwa: January 23rd, 2023

Na. Lina Sanga

Wilaya ya Njombe kupitia Halmashauri zilizopo chini ya Wilaya  hiyo imekusudia kukusanya mapato kwenye vyanzo vya ndani kwa asilimia 100 ifikapo juni,2023 na kutatua kero zinazowakabili wananchi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020-2025,kwa kipindi cha nusu mwaka kwenye kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo,kilichofanyika jana katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe.

Mhe. Kissa amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Wilaya ya Njombe imekusudia kukusanya Bil. 13.12 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani vilivyopo kwenye Halmashauri tatu zilizo chini ya Wilaya ya Njombe, ambapo Bil. 5.7 kukusanywa katika vyanzo vya ndani vya mapato katika Halmashauri ya Mji Njombe,Bil. 3.7 kukusanywa katika  vyanzo vya ndani vya mapato katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Bil. 3.5 kukusanywa katika vyanzo vya ndani vya mapato katika Halmashauri ya Mji Makambako.

Amesema kuwa, hadi kufikia desemba 31,2022 Wilaya ya Njombe imefanikiwa kukusanya mapato ya ndani Bil. 5.93 sawa na asilimia 45.3 ya lengo ambapo katika Halmashauri ya Mji Njombe jumla ya Bil. 2.98,Halmashauri ya Mji Makambako imekusanya Bil. 1.49 na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ni Bil. 1.46.

Aidha amebainisha Wilaya hiyo imefanikiwa kutoa mikopo ya asilimia 10 ka Vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri,ambapo jumla ya Mil. 957.3 zimetolewa  kwa vikundi 106 vya wanawake na vijana na 24 kwa watu wenye ulemavu.

Ameongeza kuwa,Wilaya ya Njombe imeendelea kutekeleza  miradi miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye Halmashauri zake, ambapo kwa kipindi cha julai hadi desemba 2022,Wilaya ya Njombe imetekeleza miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 62 kwa ajili ya kidato cha kwanza kwa mwaka 2023,yenye thamani ya Bil. 1.24 ambapo katika Halmashauri ya Mji Njombe jumla ya madarasa 26 yenye thamani ya Mil. 520 yalijengwa na yanatumiaka,Halmashauri ya Mji Makambako jumla ya madarasa 21 yenye thamani ya Mil. 420  yamejengwa na yanatumika na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe madarasa 15 yenye thamani ya Mil. 300 yamejengwa na yanatumiaka.

Pia ameongeza kuwa, Wilaya ya Njombe imepokea Bil. 1.4 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya tatu za Sekondari za wasichana ,ambapo Halmashauri ya Mji Njombe imepokea jumla ya Mil. 470,Halmashauri ya Mji Makambako imepokea jumla ya Mil. 470 na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Imepokea jumla ya Mil. 470.

Ametoa shukurani kwa Serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya elimu  pamoja kuongeza bajeti ya Wakala wa barabara Vijijini na Mijini (TARURA) ,kwani kupitia ongezeko hilo matengenezo ya barabara yanafanyika kwa wakati na kupunguza kero kwa wananchi.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa